Yemi Eberechi Alade amezaliwa tarehe 13 mwenzi 3 mwaka 1989 ni mtoto
wa tano katika familia ya watoto saba, elimu yake amepata katika shule
ya St. Saviour British primary, kisha akasoma sekondari ya Victory
Grammar school huko lagos na baadaye alichukua shahada yake ya geografia
katika chuo kikuu lagos.
Alade alianza maswala ya muziki mwaka 2005 pale alipokuwa katika
kundi la muziki lililoitwa Noty spices kipindi akifanya mukizi kama
kundi hakusikika sana mpaka pale ambapo alishanda katika shindano la
Peak Talent show mwaka 2009.Mwaka 2012 alisainiwa katika lebo ya Effyzie
music group na alitoa nyimbo yake ya kwanza inayoitwa Ghen Ghen Love
ilifanya vizuri kiasi chake huko kwao nchini Nigeria.
2013 mwishoni ndiyo mwaka ambayo msanii huyu alianza kupata airtime
sana katika nchi za Africa, ulaya na Marekani. Alitoa nyimbo inayoiwa
Bamboo kisha akatoa tena Jonny mwishoni mwa mwaka huo na kuteka sana
nyimbo ilifanywa chini ya SELEBOBO na kushika chati sana katika nchi
kama Tanzania, Kenya, Africa kusini, Zimbabwe, Ghana na Wingereza. Alade
aliweza kutumbuiza katika jukwaa moja na Mary J Blige pia katika tuzo
huko Nigeria mwaka 2013.
2014 Alade alishirikiana na wasanii mbalimbali kutoka Nigeria na
kushiriki katika nyimbo ya “lights” hii ni kwa ajili ya kuhimiza watotot
waende shule na wabaki shule kwa masomo pia alitoa video ya jonny
ambayo iliangaliwa mara milioni 32.
Alade aliendelea kushika chati mwaka 2015 mwishoni na kibao chake
kinachokwenda kwa jina la Na gode ambacho kimembwa kwa lugha ya
kiswahili na kingereza pia ametoa albamu moja hadi sasa.
Friday 10 November 2017
Home »
MJUE STAA WAKO LEO
» IJUE HISTORIA YA MWANAMUZIKI YEMI ALADE
0 comments:
Post a Comment